Player_logo Podcasts Community Create a Podcast
"Mimi ni Mzanzibari" na Dulla Kidume
April 01, 2012 10:53 AM PDT

"Mimi ni Mzanzibari na sitaki Muungano", anasema Dulla Kidume

Muda na Jaala
January 07, 2012 04:28 PM PST

Muda na jaala, hazina zisubiri
Mara huwa wesha, 'kawa hatunao
Lisifanywe kesho, la kufanywa leo

Zanzibar Januari 27
January 07, 2012 04:26 PM PST

Kwa kumbukumbu za mauaji ya Januari 27, 2001.
Tumesamehe.
Hatusahau!

Simchi Msicha Nchi
January 07, 2012 04:23 PM PST

Simchi kattu simchi, asiyeicha nchiye
'Siyewacha wananchi, nami simchi naye

Nikufanyeje?
December 21, 2011 08:14 PM PST

'Menijia fukara dhalili, kushakongoka, wataka nikusikize
Mararu dhoofulhali, maguuni waporomoka, wataka nikunyamaze
'Mekuja kutoka mbali, kuja lalamika, ati nikuliwaze
Haya wima tafadhali, sasa tamka, kila kitu nieleze
Kwa uradhi wa rohoyo, sema nikufanyeje!?

Kwa Nyakati Hizi
December 21, 2011 08:07 PM PST

Kwa nyakati hizi, za mwisho wa siku, tungo nayandika
Moyoni simanzi, punde ni usiku, giza litazuka
Uje uduwanzi, niwe zumbukuku, nishindwe kumbuka
Nguvu zinihizi, nifungwe vikuku, na kuporomoka
Kurasa zishafungika!

Nakumbuka
December 18, 2011 05:06 PM PST

Nakumbuka, zamani si leo. Zenji ilikuwa dola
Iliamka, mwanzo wa mawiyo, wengine walipolala
'Lihishimika, na wengi wao, ili na muala
Leo hii wapi!?

Kwa nini Wakakupiga?
December 18, 2011 04:46 PM PST

Mwanangu unanijia, hali unatiririka, damu muili mzima
Tumboni ninaumia, ini linanikatika, moyo wapwita wauma
Lipi limekutokea, shenzi walonaalika, washakupiga kwa vyuma!?
Kwa nini wakakupiga?

Zanzibar Yangu Siuoni Mfanowo
December 17, 2011 07:13 AM PST

"Hushika kalamu kuiandika sifayo
Humalizika wino sijayesha manenoyo
Vitabu vi tele: Ulaya, Asia na Amerika zitajazo hadhiyo
Huja mawiyo, kaja machana, yakaja machweyo
Ela kamwe sishi kuitaja hishimayo"

Kwa Jina la Zanzibar
December 17, 2011 05:55 AM PST

Kwa jinalo wewe, tungo naiandika, na kuikariri
Nataka ujuwe, ndiwe msifika, ndiwe wangu huri
Lolote naliwe, sitakukanuka, sitakughairi
Kila kitu wewe, uliyetukuka, Mama Zinjibari!

Nyumbani Oo Nyumbani!
December 14, 2011 04:54 AM PST

Nyumbani oo nyumbani, kwetu ninakukumbuka
Gizani humu gizani, machozi yamiminika
Kwa nini hivi kwa nini, kwetu miye nikauka?

Haijawa ya kuvunda...
November 25, 2011 11:33 PM PST

Ilipovunjika, isikandike, sasa itakandika
Ilipokatika, isiungike, sasa itaungika
Lipochanjagika, isikandike, sasa itakandika
Yetu sio ya kuvunda, ina ubani!

Naota
November 25, 2011 11:23 PM PST

Naota ni mkoloni, naitawala Ulaya
Britini, Jarumani, Uswidi na Rumania
Zote zimo mikononi, ninazo nazikalia

Uskoti na Udeni, Ureno hadi Rusiya
Wapo pangu maguuni, amri wanangojea
Nawambia: “Piganani!” nao vitani wangia

Ni Yeye
November 25, 2011 11:18 PM PST

Ni yeye nimuwazaye, munamo fikira zangu
Ndiye mwezi nimwonaye, ang’araye kwenye mbingu
Na nyota aongozaye, dira ya safari yangu
Ni yeye ndiye mwenyewe!

Tunao huu Tunao!
November 25, 2011 11:09 PM PST

Tunao huu tunao, twendanao polepole
Wala hatutaki mbao, matawi wala shinale
Tutakalo twende nao, tuubwage chalechale
Na tutawatenda ja vile, kulinda wajifanyao

Next Page